Sunday 5 March 2017

MTI WENYE UMRI MREFU ZAIDI DUNIANI WAGUNDULIKA KILIMANJARO TANZANIA


Siku chache baada ya wanasayansi kubaini mti mrefu zaidi barani Afrika katika Mlima wa Kilimanjaro nchini Tanzania sasa wataalam hao wamefanya ugunduzi mwengine kuhusu mti huo.

Wataalam hao kutoka chuo kikuu cha Beyreuth Ujerumani sasa wamegundua kwamba mti huo ndio ulio na miaka mingi zaidi duniani.

Kulingana na gazeti la Mwananchi nchini Tanzania, Mtafiti wa viumbe hai na mazingira kutoka Chuo hicho Dk Andrew Hemp ameelezea sifa za mti huo ujulikanao kama Mkukusu kuwa unaweza kuishi kati ya miaka 200 hadi 300, lakini ulioonekana nchini una miaka 600.

Mti huo unapatikana katika Kijiji cha Tema wilayani Moshi, na upo katika eneo lililopo kwenye Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro (kinapa).

Dk Andrew amesema kwa mujibu wa utafiti mti huo una uwezo wa kuishi miaka hiyo kwa kutunzwa na kuhifadhiwa.


Kulingana na gazeti hilo la mwananchi ,Amesema kwamba katika utafiti walioufanya barani Afrika waligundua miti mirefu 31, lakini Mkukusu wa Moshi ndiyo mrefu kuliko yote na una umri wa miaka 600 hivi sasa ukiwa umevuka kiwango cha juu cha maisha ya miti ya aina hiyo.

Tayari Serikali imeiagiza Kinapa kuboresha miundombinu ya barabara ili kuweza kuufikia mti huo iwapo watalii watataka kwenda kuuona.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Meck Sadiki amesema mti huo utasaidia kuongeza mapato kwa kasi kwa kuwa ni kivutio kipya cha utalii ndani ya mkoa huu.

Mhifadhi Mkuu wa Kinapa, Betrita Loibok amesema agizo hilo litazingatiwa kwa kushirikiana na Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (Tanapa) ili mti huo uweze kuwa kivutio ndani na nje ya chini

ya nchi.

No comments:

Post a Comment